S H E I K H

l o a d i n g
maulid bidaa haramu

JE, MAULID NI BIDA'A? | SHEIKH ABDILAHI NASSIR

Kumekuwa na utamaduni wa muda mrefu kwa jamii za Kiislamu kufanya hafla za Maulid au Sherehe za mazazi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w). Aghalabu sherehe hizo huwajumuisha waislamu bila kujali tofauti zao za kiitikadi na kumsifu Mtume kwa namna mbalimbali.


Hata hivyo, katika jamii hizo za Kiislamu kumekuwa na mtazamo mseto juu ya uendeshaji wa maulid hizo. Wapo katika Waislamu wanaosema kuwa Maulid ni bida'a na hata kufikia kuiharamisha lakini pia wapo ambao wanatilia mkazo juu ya uendeshaji wa hafla hizo na kila undi likiwa na hoja zake.


Sheikh Abdilahi Nassir alipata fursa ya kutoa hoja zake juu ya suala hili lakini pia kuangazia nafasi ya sherehe za maulid kwenye jamii za Kiislamu...

  • Jun 28, 2024
hija makkah

MAANA YA HIJA | SHEIKH ABDILAHI NASSIR

Ibada yaHija ni moja ya nguzo muhimu katika Uislamu ambapo, kila Muislamu anatarajiwa kuhiji angalau mara moja katika maisha yake ikiwa ana uwezo.


Hata hivyo, uzoefu unaonesha kumekuwa na mitazamo tofauti juu ya namna watu wanavyoichukulia ibada hiyo. Kwa mfano, wapo wanaichukulia ibada hiyo katika mtazamo wa kiroho tu lakini pia wapo ambao wanaitazama ibada ya hija kama fursa ya kupitisha na kuendesha ajenda nyingine kwa maslahi mapana ya Uislamu...


Sheikh Abdilahi Nassir, alitoa hoja zake juu ya namna watu hususani Waislamu wanavyopaswa kuichukulia ibada ya hija.

  • Jun 28, 2024
shia hadith abdilahinassir

SHIA NA HADITHI

Hadithi, ni moja kati ya mambo muhimu ambayo yanatoa muongozo kwenye mambo mbalimbali ndani ya Uislamu.


Hata hivyo, kumekuwa na tuhuma zimekuwa zikielekezwa kwa Waislamu wa madhehebu ya Shia Ithana-Asheri juu ya kuwa na mtazamo tofauti juu ya namna wanavyozitazama hadithi.


Sheikh Abdilahi Nassir alipata fursa ya kuandika kitabu 'Shia na Hadithi' akijibu na kutolea hoja juu ya suala hili.

  • Jun 28, 2024
maulid bida haramu abdilahinassir

MAULID SI BIDA, SI HARAMU

Kumekuwa na utamaduni wa muda mrefu kwa jamii za Kiislamu kufanya hafla za Maulid au Sherehe za mazazi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w). Aghalabu sherehe hizo huwajumuisha waislamu bila kujali tofauti zao za kiitikadi na kumsifu Mtume kwa namna mbalimbali.


Hata hivyo, katika jamii hizo za Kiislamu kumekuwa na mtazamo mseto juu ya uendeshaji wa maulid hizo. Wapo katika Waislamu wanaosema kuwa Maulid ni bida'a na hata kufikia kuiharamisha lakini pia wapo ambao wanatilia mkazo juu ya uendeshaji wa hafla hizo na kila undi likiwa na hoja zake.


Sheikh Abdilahi Nassir alipata fursa ya kujibu na kueleza hoja zake juu ya suala hili la Maulid.

  • Jun 28, 2024
shia quran abdilahinassir

SHIA NA QURAN

Uislamu unaundwa na viungo kadhaa, miongoni mwavyo ni kuamini kwamba hapana Mola apasaye kuabudiwa isipokuwa Allah (S.W.T) na Muhammad (s.a.w.w) ni mtume wake mwisho miongoni mwa mitume walioagizwa kutulingania.


Hata hivyo, ni jambo la wazi kwamba sasa Uislamu umegawanyika kiitikadi hususani kwenye eneo la uongozi baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w). Hali imepelekea kila kundi katika Uislamu kujiona kuwa ni sahihi zaidi kuliko lingine na ndani yake kukatokea kushutumiana kwenye mambo mbalimbali. Kwa mfano, kumekuwa na hoja kutoka upande mmoja ukidai kwamba wafuasi wa Maimamu 12 (Shia Ithna-Asheri) wana Qur'an (msahafu) wao tofauti na unaotumiwa na jamii nyingine za Kiislamu.


Je, hoja hiyo ina ukweli kiasi gani?, Sheikh Abdilahi Nassir alipata fursa ya kuandika kitabu 'Shia na Qur'an' akijibu na kutolea hoja juu ya suala hili.

  • Jun 28, 2024