S H E I K H

l o a d i n g

Book

SHIA NA TAQIYA

Taqiya, ni neno la kiarabu ambalo linatafsiriwa kama 'kinga' katika lugha ya kiswahili. Katika maneno mengine, ni kusema kwamba unaficha uhalisia fulani ili usidhurika.Taqiya imekuwa ikifanyika tangu wakati wa Mtume Muhammad (s.a.w.w). Wakati ambapo Uislamu ulikuwa katika hali ya uchanga, ili wabidi Waislamu wafundishane katika hali ya kujificha, walikuwa wakifanya hivi kujiepusha na madhara ambayo wangeyapata kutoka kwa maquraish wa Makkah. Kuna visa vingi tu vya maswahaba ambao iliwabidi wakubaliane na batili na kuicha haki huku wakiendelea kuamini katika haki ili kulinda usalama wao.


Hata hivyo, kwa muda sasa pamekuwa pakitengenezwa tuhuma dhidi ya Waislamu wa madhahebu ya Shia Ithna-Asheri kwamba wao sio Waislamu (wanafanya taqiya) ni wanafiki.


Sheikh Abdilahi Nassir alipata fursa ya kuandika kitabu 'Shia na Taqiya' akijibu na kutolea hoja juu ya suala hili na kubainisha msimamo wa Mashia juu ya habari ya taqiya.

more Book
shia hadith abdilahinassir

SHIA NA HADITHI

shia quran abdilahinassir

SHIA NA QURAN